QR Code: cBKPpogJ4L

Ripoti hii inawasilisha udhaifu, mahitimisho, na mapendekezo ya taarifa 14 za Ukaguzi wa Utendaji uliofanywa kwa mwaka wa fedha 2022/23. Ukaguzi wa utendaji ulihusisha udhibiti wa usambazaji wa mbolea, vifaa tiba, elimu ya ufundi na mazao ya biashara, usimamizi wa fukwe, rasilimali za uvuvi, mipango miji na uagizaji wa bidhaa za petroli, upatikanaji wa huduma za afya ya akili, urejeshaji wa mikopo, utoaji wa usaidizi kwa wachimbaji wadogo wadogo, utekelezaji wa mipango ya maboresho ya tabia za wafungwa, usimamizi na ufuatiliaji wa watoa huduma za bima, kukuza, kufuatilia na kutathmini uwezo wa wafanyakazi katika sekta ya umma.